11/05/2010

Matokeo ya Uchaguzi Tanzania

Matokeo ya uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa.

 
Walio piga kura 8,626,283 – 42.84%

Kura zilizoharibika – 227,889 – 2.64%
 
Kura halali – 8,393,394 – 97.36%

Idadi ya kura na asilimia kwa kila chama ni kama ifuatavyo:
 
1. APPT Maendeleo - 96,933 – 1.12%

2. Chama Cha Mapinduzi – 5,276,827 – 61.17%

3. CHADEMA – 2,271,941 – 26.34%

4. CUF – 695,667 – 8.06%
5. NCCR Mageuzi – 26,388 – 0.31%
 
6. TLP – 17,482 – 0.20%
 
7. UPDP – 13,176 – 0.15%
 

10/30/2010

CCM Yahitimisha Kampeni Jangwani Leo. JK awasuta wanao beza maendeleo


 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete, akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake, wakati akihitimisha mikutano yake ya kampeni kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam leo jioni Oktoba 30, 2010. Uchaguzi mkuu wa Tanzania utafanyika Jumapili Oktoba 31, 2010.





Wafuasi wa CCM wakishangilia hotuba ya mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete wakati akihitimisha mikutano yake ya kampeni kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam Oktoba 30, 2010.

- Asema hakuna mchawi wakati huu!
- Asema hakuna haja ya kuiba gari la vipodozi na kujaza makaratasi ya kura, CCM itashinda tu!

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi amewashukuru wana CCM leo kwenye hutuba yake ya kufunga kampeni kwa kukipigania Chama chake na kuwaandalia mapokezi mazuri kipindi chote cha kampeni.

Amesema ametembea nchi nzima na kufanya mikutano mikubwa kwenye majukwaa 280, na ile ya kusimama njiani na ya ndani 420 nchi nzima.

Aliongeza CCM ni chama pekee ambacho kimezunguka Tanzania nzima na kuzungukia majimbo yote 330 ya uchaguzi Tanzania nzima. Alisema yeye akishirikiana na mgombea mwenza Dr. Gharib Bilal wamezunguka kote ambako mmoja wao alishindwa kutembelea, mwingine alisaidia. Alisisitiza kuwa kuna baadhi ya maeneo mengine nchini ambapo yeye na mgombea mwenza walipita na kufanya mikutano mikubwa ya kampeni.

Akimshukuru Mama Salma kwa kuendesha kampeni kubwa kwa ajili ya Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Kikwete alisema Mama Salma ameonyesha ujasiri mkubwa na uwezo mkubwa wa kunadi sera za chama chake.

"Japo wapinzani hawakupenda jitihada hizo, lakini wao wengine hawana wake (hawajaoa), wengine wanataka kuingia Ikulu na "ma first lady" wa wenzao (wake za watu). Nasema Mungu atunusuru na viongozi kama hao". Alisema Kikwete huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu waliofurika viwanja vya Jangwani.

Mheshimiwa Kikwete alichukua nafasi hiyo pia kuelezea wana CCM na wananchi waliohudhuria mkutano huo mkubwa kuwa wakati anazunguka mikoani, aliwaeleza wananchi sera na malengo ya CCM na wao walikubali na kumuhakikishia watachagua tena CCM iendelee kuongoza.

Mwishoni Mheshimiwa Kikwete aliwaomba Watanzania wote kupitia mkutano huo wachague Chama Cha Mapinduzi kwani ni waaminifu na wanatoa ahadi zinazotekelezeka. "Hakuna chama kingine kama CCM" alisema.

"Mzee Mkapa ameeleza maneno ya busara, uchaguzi huu usitugawe...wanataka kuingia Ikulu kwa ngazi ya maiti za Watanzania? Tuwaepuke viongozi hao. Msiwasikilize, achaneni nao" Kikwete alisisitiza.

Aliahidi Watanzania kuwa yeye na Dkt Bilal wakichaguliwa, watatumia uzoefu wao wa miaka mingi kwenye utumishi wa umma, kulinda amani na utulivu, na kuendeleza maendeleo ya taifa la Tanzania.

Alisisitiza serikali yao itajali maslahi ya watu wote, wenye ulemavu, watoto, vijana, wazazi, wazee na watu wa matabaka yote. Kama serikali ya CCM inavyovyofanya sasa. Pia aliwasihi Watanzania wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura siku ya uchaguzi kwani ni haki yao ya msingi na ya kikatiba.

Mkutano wa Kampeni Jangwani - Mzee Ruksa na Mkapa wampigia chapuo JK

Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa akimpongeza Rais Dr.Jakaya Mrisho Kikwete katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam.





Wakati mkutano wa kampeni wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Kikwete ukiendelea viwanja vya Jangwani, marais wastaafu wa awamu ya pili na ya tatu wamemnadi Mheshimiwa Kikwete leo.

Akimnadi Mheshimiwa Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mheshimiwa Benjamin William Mkapa amewasuta waliosema amemtelekeza Rais Kikwete na kampeni zake. Alisema kamwe hawezi kumuacha Rais Kikwete kwani uongozi wake unasifika dunia nzima.

Mheshimiwa Mkapa alisema amemjua Rais Kikwete na kufanya naye kazi muda mrefu tangu akiwa mkuu wa wilaya yake. Walifanya kazi kwa pamoja kuukimbiza mwenge na kuukabidhi wilaya inayofuata.

Mheshimiwa Mkapa alisema anatambua kuwa Rais Kikwete ana dhamira ya kuongoza, anaijua hali halisi ya nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kwa kila hali. Hakuna mgombea kama yeye. "Wagombea wengine wanaitana mmoja ni Kilimanjaro mwingine ni kichuguu. Mimi nasema wote ni kokoto!"

 
Umati wa wanachama wa CCM katika viwanja vya jangwani waliohudhuria mkutano wa kilele cha kampeni jijini Dar es Salaam leo mchana.

Umati wa wanachama wa CCM katika viwanja vya jangwani waliohudhuria mkutano wa kilele cha kampeni jijini Dar es Salaam leo mchana.

Umati wa wanachama wa CCM katika viwanja vya jangwani waliohudhuria mkutano wa kilele cha kampeni jijini Dar es Salaam leo mchana.
Alisema anasikitika kuwa hakupata nafasi ya kwenda Zanzibar kuwasihi waendeleze amani na utulivu wakati wa uchaguzi. Alisisitiza kuwa anaunga mkono uamuzi wa wazanzibari wa kuunda serikali ya muungano, lakini anaamini kuwa ni CCM pekee ndiyo itakayoweza kuongoza na kuendeleza mapinduzi ya 1964.

Mkutano wa Kampeni Jangwani, Dar es salaam








Baada ya siku 69 za kampeni kutetea kiti chake cha urais, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo anahitimisha kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani wilayani Ilala, Mkoa wa Dar es salaam.

Akitoa utangulizi kabla ya Mheshimiwa Kikwete kuhutubia maelfu ya wana CCM waliohudhuria mkutano huo, Katibu Mkuu wa CCM Lt. Mstaafu Yusuph Makamba alisema Mheshimiwa Kikwete amefanya kampeni safi iliyojumuisha mikutano 330 nchi nzima, na alisafiri kwa barabara na anga umbali wa kilometa 22,000 nchi nzima.

Mheshimiwa Kikwete anategemewa kuhutubia mkutano huu mkubwa muda mchache kutokea sasa, baada ya katibu wa chama kuongea na mgombea mwensa Dr. nilal Hutuba hiyo itarushwa moja kwa moja vituo vya Start TV na TBC na kwenye mtandao itarushwa moja kwa moja na VIZA TV kupitia habaricom.

10/29/2010

Mkutano wa Mgombea Urais wa CCM na waandishi wa habari - Picha













Mazungumzo ya Mheshimiwa Kikwete na waandishi wa habari

Baadhi ya wageni waalikwa wakisikiliza mazungumzo ya Mheshimiwa Kikwete na waandishi wa habari


Wawakilishi wa TBC Susan Mongy na ITV Masatu wakiwa kwenye mazungumzo na Mheshimiwa Kikwete leo

Awamu ya pili ya maswali ya wawakilishi wa vituo vya televisheni mbalimbali nchini kwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrsiho Kikwete imeanza wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari.

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa ni yale kuhusiana na maboresho kwenye sekta ya afya na ahadi za mgombea kwa Watanzania kuhusiana na afya, manung'uniko kuhusu utoaji wa haki katika mahakama, tatizo la rushwa na jinsi mgombea atakavyoendesha mapambano dhidi ya rushwa.

Mwisho Mheshimiwa Kikwete alitoa rai kwa Watanzania wote kutumia nafasi waliyopewa kikatiba ya kuchagua kiongozi wanayemtaka. Pia aliongeza kuwa Watanzania tuna historia ya amani duniani kote haswa kipindi cha uchaguzi. Aliwasihi watanzania kutofuata muelekeo wa kuchagua viongozi kwa misingi ya dini kwani kwa kufanya hivyo, itaweza kuleta migogoro nchini baada ya uchaguzi.

Mazungumzo ya Mheshimiwa Jakaya Kikwete na waandishi wa habari Leo

Mheshimiwa Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na wawakilishi wa vituo mbalimbali vya televisheni nchini usiku wa leo


Baadhi ya waalikwa wakisikiliza mazungumzo ya baina ya mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM na waandishi wa habari usiku wa leo tarehe 29.10.2010

Mheshimiwa Kikwete akiingia kwenye ukumbi wa Arnaoutoglou jijini Dar es salaam kuanza mazungumzo na waandishi wa habari leo.

Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na waandishi wa habari leo tarehe 29.10.2010


Mazungumzo ya mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na waandishi wa Habari yanaendelea kwenye ukumbi wa Arnautoglou kuanzia saa mbili usiku hadi saa nne usiku.

Baadhi ya maswali yaliyo ulizwa na wawakilishi wa vituo mbalimbali vya televisheni ni:
- Kuhusu mtazamo wake kuhusiana na wizi wa kura vituoni wakati wa upigaji kura.
- Matokeo ya tafiti mbalimbali  zinazoashiria matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2010,
- Ajira kwa vijana,
- Maendeleo kwenye sekta ya elimu,
- Halihalisi ya nchi katika mizunguko yake ya kampeni nchi nzima,
- "Legacy" atakayowaachia watanzania pindi atakapomaliza muda wake wa uongozi
- Aliwezaje kuwanadi wagombea ubunge na udiwani wa CCM waliokuwa na kesi mbalimbali na shutuma mahakamani
- Na mwisho ni sura ipi ya serikali atakayoiunda pindi akifanikiwa kuendelea kuongoza ambapo atamuachia kiongozi mwingine tayari kuanza safari ya mwaka 2025 ya malengo ya milenia.

Awamu ya kwanza ya maswali imemalizika, na sasa awamu ya pili ya maswali inaanza.

Mazungumzo haya yanarushwa moja kwa moja na vituo vyote vya televisheni. Pia Radio Clouds na Radio Uhuru wanarusha mazungumzo haya mojakwamoja.

VIZA televisheni ya kwenye mtandao wa internet kupitia HabariCom inarusha mazungumzo haya moja kwa moja kwenye mtandao wa internet, pamoja na kurasa zote za jamii za jakayakikwete2010 (social media sites) za twitter, facebook na blogspot.