10/29/2010

Mazungumzo ya Mheshimiwa Kikwete na waandishi wa habari

Baadhi ya wageni waalikwa wakisikiliza mazungumzo ya Mheshimiwa Kikwete na waandishi wa habari


Wawakilishi wa TBC Susan Mongy na ITV Masatu wakiwa kwenye mazungumzo na Mheshimiwa Kikwete leo

Awamu ya pili ya maswali ya wawakilishi wa vituo vya televisheni mbalimbali nchini kwa mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrsiho Kikwete imeanza wakati wa mazungumzo yake na waandishi wa habari.

Baadhi ya maswali yaliyoulizwa ni yale kuhusiana na maboresho kwenye sekta ya afya na ahadi za mgombea kwa Watanzania kuhusiana na afya, manung'uniko kuhusu utoaji wa haki katika mahakama, tatizo la rushwa na jinsi mgombea atakavyoendesha mapambano dhidi ya rushwa.

Mwisho Mheshimiwa Kikwete alitoa rai kwa Watanzania wote kutumia nafasi waliyopewa kikatiba ya kuchagua kiongozi wanayemtaka. Pia aliongeza kuwa Watanzania tuna historia ya amani duniani kote haswa kipindi cha uchaguzi. Aliwasihi watanzania kutofuata muelekeo wa kuchagua viongozi kwa misingi ya dini kwani kwa kufanya hivyo, itaweza kuleta migogoro nchini baada ya uchaguzi.

No comments:

Post a Comment