8/31/2010

Marlow aongoza wasanii wa kizazi kipya na kuwapagaisha wana CCM Mbeya Mjini

Marlow akiondoka kiduku na vuvuzela wakati akitumbuiza wana CCM na wimbo wake wa Pipi CCM remix.


Bushoke na Hafsa Kazinja (chini) nao walikuwepo kwenye kundi hilo la wasanii. Maelfu ya wana CCM waliofurika kwenye uwanja wa Sokoine waliburudika sana na nyimbo za wasanii hawa.

Vikundi mbalimbali vya wasanii vimepamba Mkutano wa Kampeni ya Mgombea Urais wa CCM Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete mjini Mbeya jioni hii lakini Marlow na wimbo wake Pipi Remix CCM umefunika!
Wengine waliokwisha kutumbuiza hadi sasa ni Hafsa Kazinja, Bushoke, Inspekta Harun. Ambao wanatarajiwa kupanda kwenye stage baada ya Marlow ni kikundi cha vichekesho cha Original Comedy.

Mojawapo ya vivutio vilivyowachanganya wana CCM uwanjani hapa ni uwezo mkubwa wa muimbaji huo kuimba bila vyombo mashairi ya wimbo wake mpya ambao umetamba sana kwenye kampeni hii ya Mheshimiwa Kikwete.

"Pipi...move out of the way, hatukuja kupoteza time, tunarudi tena kwa kishindo na Jakaya ndiyo Rais. Haloo sasa tuungane tushikamane, kwa pamoja tusonge mbele CCM ni Zaidi"
Blog hii ya kampeni inasubiri maneno kamili ya mwimbo huu ambao unapatikana kwenye CD ya mkusanyiko wa nyimbo za kampeni ya CCM za wasanii wa kizazi kipya. Wasanii wengine wanaosikika kwenye albamu hii mpya ya CCM ni Mheshimiwa Temba na Chege na wimbo wao wa "Mkono mmoja CCM remix" Diamond na mwimbo wake wa "Chagua CCM" wenye midundo ya "Mbagala" na msanii maarufu kutoka nchi jirani Kidumu.

No comments:

Post a Comment