8/30/2010

Mkutano wa Kampeni Mbalizi Mbeya Vijijini: Wanachama 367 Chadema waingia CCM

Aliyekuwa Katibu wa Chadema akionyesha kadi za chama hicho alizozikabidhi CCM baada ya kutangaza rasmi kuingia CCM akiongozana na viongozi wengine saba na wanachama wengine zaidi ya 300.



Aliyekuwa Katibu wa Wilaya ya Mbeya Vijjijini na hatimaye Katibu wa Mkoa wa Mbeya Chadema Ipyana Seme ameingia Chama Cha Mapinduzi akiongozana na wengine 366 wa CHADEMA.
Akishangiliwa na umati mkubwa wa watu uliofika kumsikiliza Mheshimiwa Kikwete, Seme alitangaza sababu kubwa tatu zilizomfanya kuhamia CCM ikiwa ni pamoja na kuchoshwa na siasa za ukabila, uongo na kufumbia macho mazuri yaliyofanywa na CCM.
“Leo naingia CCM na nimeongozana na viongozi saba ngazi ya Wilaya na jumla ya wanachama 367” Seme alisema huku akishangiliwa na wana CCM kwa vigelegele.
Viongozi waliotajwa kuingia CCM ni wale walio kwenye ngazi zifuatazo: Mwenyekiti wa baraza la wanawake mkoa, Mweka hazina wa wilaya, Mwenyekiti baraza la wazee, Mjumbe wa halmashauri kuu ya wilaya, Mshauri wa wanawake wilaya na mwenyekiti wa vijana wa wilaya.
Seme aliwatambulisha viongozi hao waliofika jukwaani na kukabidhiwa kadi zao na Mwenyekiti wa CCM Taifa na Mgombea Urais Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Mwisho Seme alitoa ujumbe kwa mgombea urais kupitia Chadema “Mpelekeeni kadi hizi (za Chadema) kwenda Ikulu bado kwa Mheshimiwa Slaa….bai bai”

1 comment:

  1. jamani chadema bado. wanafanya siasa nyepesi nyepesi. CCM 2010 USHINDI LAZIMA

    ReplyDelete