8/31/2010

Ze Original Comedy ndani ya Mkutano wa Kampeni Mbeya Mjini

Ni shangwe na burudani za hali ya juu hapa Mjini Mbeya kwenye uwanja wa Sokoine ambapo maelfu ya washabiki wa CCM wamefurika kuhudhuria Mkutano wa Kampeni ya Mheshimiwa Kikwete.
Sasa hivi walioko jukwaani ni kundi la Original Comedy na wameshaigiza nyimbo maarufu ya Komba "wembe ni ule ule", pia wameigiza "FM academia wazee wa ngwasuma, na sasa wanaimba Pembe la Ng'ombe.
Pia kundi hilo limetoa ujumbewa pongezi kwa wananchi wa Mkoa wa Mbeya kipindi kwa kujitokeza kwa wingi kumsikiliza Mgombea Urais wa tiketi ya CCM, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Wasanii hawa wataendelea kutoa burudani mara baada ya Mheshimiwa Kikwete kuzungumza na wananchi.

No comments:

Post a Comment