8/31/2010

Mkutano wa Kampeni, Rungwe








Mapokezi makubwa yamemkaribisha Mheshimiwa Kikwete alipowasili Rungwe kwenye mkutano wake wa pili wa kampeni kwa siku ya leo.

Mapokezi hayo yaliambatana na mapikipiki 50 yaliyomlaki njia panda na kumsindikiza hadi kwenye eneo la mkutano uliofanyika kwenye Uwanja wa Tandale hapa Rungwe.

Kabla ya Mheshimiwa Kikwete kuzungumza na umati huo mkubwa wa watu, wabunge wawili wa Rungwe walizungumza ambao wote ni mawaziri; Mheshimiwa Mark Mwandosya na Mheshimiwa David Mwakyusa.

Kwenye salamu zao za shukrani, mawaziri hao wawili walimshukuru Mheshimiwa Kikwete kwa imani yake kwao kuwapa majukumu ya kuongoza wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Naye Mwenyekiti wa CCM Taifa na Mgombea wa Urais CCM Mheshimiwa Kikwete akizungumzia mafanikio ya Chama cha Mapinduzi kwenye upande wa afya alisema yeye na Mheshimiwa Mwakyusa wamebuni mikakati mingi zaidi ya kukabiliana na Malaria ikiwa ni pamoja na kugawa vyandarua viwili kila kaya Tanzania nzima.
Pia Mwenyekiti alichukua nafasi hii kuelezea mafanikio mbalimbali ya utekelezaji wa ilani ya CCM na mengine yaliyoongezeka kwa miaka mitano ijayo.
Mwisho kabisa Mheshimiwa Kikwete aliwaombea kura madiwani na wabunge wa CCM kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa oktoba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment