8/30/2010

Ratiba ya Kampeni za Mheshimiwa Kikwete Leo - Jumatatu 30/8/2010

Kampeni za Mgombea wa Urais kupitia CCM, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo zimeingia siku ya kumi na ziko Mkoa wa Mbeya. Kwa mujibu wa ratiba, Mheshimiwa Kikwete atahutubia Mkutano wa Kampeni Vwawa Wilaya ya Mbozi na kuelekea Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini. Pia Mheshimiwa Kikwete atasimama Mlowo kusalimiwa wananchi kabla hajaendelea Mbalizi.
Mheshimiwa Kikwete atafanya Mikutano wa Kampeni Mkwajuni na Makongolosi wilayani Chunya kabla hajaendelea Chunya Mjini kukutana na Wazee wa Chunya.

1 comment: