9/24/2010

Kampeni za Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete Leo

Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameanzia kampeni zake leo mkoani Manyara, wilaya ya Ngorongoro, Loliondo.

Baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni Ngorongoro, msafara wa Mheshimiwa Kikwete utaelekea Mkoani Mara ambapo atafanya mkutano wa kampeni Mugumu na Shirati.

Kutokea hapo atasimama maeneo  ya Ingri kusalimiana na wananchi na kufanya mkutano wa kampeni kabla ya kuendelea Utegi na hatimaye Tarime Mjini.

Pia akiwa Tarime Mjini, Mheshimiwa Kikwete anatarajiwa kufanya kikazo za wazee wa Tarime, ambapo itakuwa ndio mkutano wake wa mwisho wa kampeni kwa siku ya leo, ambapo atakuwa amehutubia Mikoa ya Manyara na Mara.

No comments:

Post a Comment