9/24/2010

Mkutano wa Kampeni Tarime: Wana Tarime wamkubali JK: Picha

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia maelfu ya wananchi wa mji wa Tarime uliuoko katika mkoa wa Mara katika mkutano wa kampeni.


 Kijana mmoja ambaye ni mshabiki wa Chama Cha Mapinduzi katika mji wa Tarime aliamua kujichora mwili wake wote kwa rangi ya kijani na manjano wakati wa mkutano wa kampeni uliohutubiwa na Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Mgombea wa Urais kupitia chama hicho Mheshimiwa Jakaya Kikwete akimtambulisha mgombea ubunge wa jimbo la Tarime ndugu Nyambare Nyangili wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika mji wa Tarime

No comments:

Post a Comment