9/16/2010

Mkutano wa Kampeni Bomang'ombe - Mapokezi ya JK yanatisha, Mbunge ammwagia sifa JK

Kina mama wana CCM wa Hai kwenye uwanja wa mkutano wa Bomang'ombe wakishangilia wakati msafara wa Mheshimiwa Kikwete ukiwasili uwanjani Bomang'ombe.

Maelfu ya wananchi waliofurika kwenye uwanja wa mkutano wa Bomang'ombe kumsikiliza Mheshimiwa Kikwete alipowasili kwenye mkutano mkubwa wa kampeni.

Mheshimiwa Kikwete akipokelewa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Hai kabla ya kuhutumia maelfu ya watu waliofika kumsikiliza kwenye mkutano wake mkubwa wa kampeni Bomang'ombe

Mheshimiwa Kikwete akisalimiana na vijana wa Kwasadala ambapo aliwashangaza wengi aliposhuka na kujichanganya na wananchi wa mahali hapo.

Msafara wa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete sasa umeingia Bomango'mbe Wilaya ya Hai na kulakiwa na mapokezi ya kutisha.
Msafara huo uliotokea Masama na old Moshi, uliwasili uwanja wa mkutano majira ya saa 7:40 ukisindikizwa na magari na pikipiki kuanzia barabara kuu ya Moshi-Arusha.

Kabla ya kuwasili Bomang'ombe, msafara wa Mheshimiwa Kikwete ulisimama Kwasadala ambapo mgombea huyo alishuka na kuanza kusalimiana na wananchi waliokuwa wanamsubiri kwa shauku kubwa.

Kijana mfanyabiashara ndogondogo hapo Kwasadala alikiri kuwa hawakutegemea kumuona Mheshimiwa Kikwete na kumshika mkono, na kikubwa zaidi ni pale aliposhuka na kujichanganya na wakazi wa eneo hilo.

"Si unaona, huyu sio bishoo kabisa, ni mtu wa watu, ni mtu wa kujichanganya na huyu ndio mwenye dola. Wengine hawajashika dola lakini hawajichanganyi na sisi, ubishoo mtupu!" Alimaliza kijana huyo aliyejulikana kwa jina moja tu, Sadati.

Naye mgombea Ubunge wa Jimbo la Hai kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Fuya Kimbita alimmwagia sifa nyingi Mheshimiwa Kikwete kabla ya kuanza hotuba yake ya kampeni.

Alisema mafanikio ya wazi yamepatika Wilaya ya Hai katika kipindi cha miaka mitano iliyopita hususan kwenye upande wa elimu ambapo ufaulu wa wanafunzi wa sekondari umeongezeka kutoka 42% mwaka 2005 hadi 70%. Shule mpya za Sekondary za kata 18 zimejengwa na hivyo kufanya idadi ya shule za sekiondari kufikia 43.

Mafanikio mengine yaliyopatikana ni kwenye upande wa ujenzi wa barabara (miundombinu) ambapo barabara zote zimekarabatiwa kwa kiwango cha kupitika. Mengine ni upatikanaji wa maji safi na salama, ruzuku kwenye upande wa kilimo, upanuzi wa hospitali na upatikanaji wa huduma za afya ambapo Wilaya ya Hai sasa itakuwa na hospitali pacha kwa jitihada za serikali ya CCM.

No comments:

Post a Comment