9/29/2010

Mkutano wa Kampeni Tabora Mjini: Mapokezi ya JK yatia fora! Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi wafurika


Umati wa wananchi wa Tabora Mjini wamefurika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi leo kumsikiliza Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipofanya mkutano wa kampeni leo tarehe 29.9.2010


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Tabora Mjini kwa Mkutano wa kampeni jioni hii na kuteka umati wa watu wa Tabora.

Huu ni mkutano wake wa tatu kwa siku ya leo na kwa mkoa huu wa Tabora ambapo asubuhi alianzia Bukene, Nzega na sasa Tabora Mjini.

No comments:

Post a Comment