9/13/2010

Maelfu wampokea JK Kwashemshi

Wanakijiji wakitokea kwenye mashamba ya chai wakishangilia CCM juu wakati msafara wa Mheshimiwa Kikwete ukipita kuelekea Bumbuli leo jioni.
Wananchi waliokuwa pembezoni wakimsikiliza Mheshimiwa Kikwete kwa makini alipokuwa akisalimiana nao Kwamsheshi akielekea Bumbuli.

Mheshimiwa Kikwete akihutubia wananchi wa Kwamsheshi aliposimama kuwasalimu
Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi amesimama Kwashemshi Wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga na kulakiwa na umati mkubwa wa watu.

Mheshimiwa Kikwete alisimama Kwashemshi akitokea Korogwe kuelekea Bumbuli kwenye Mkutano wa Kampeni.

Akizungumza na wananchi hao, Mheshimiwa Kikwete alitumia nafasi hiyo kuwanadi wagombea udiwani na ubunge wa CCM.

Akimnadi Steven Ngonyani au Profesa Maji Marefu, mgombea ubunge Korogwe Vijijini Mheshimiwa Kikwete aliwaambia wananchi kwamba wamempata mtendaji na mchapakazi wampe kura zote ili ashirikiane na wengine wote wa CCM katika kuleta maendeleo.

No comments:

Post a Comment