9/26/2010

Mkutano wa Kampeni Nyanguge Wilayani Magu

Msafara wa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi taifa na Mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia chama hicho Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete umewasili Nyanguge mchana huu.

Akishangiliwa na umati mkubwa wa watu, Mheshimiwa Kikwete amewasihi wananchi wa hapo kuchagua CCM ili iweze kuendeleza kazi nzuri iliyokwisha kufanywa na chama hicho.

Alisema anayaelewa matatizo makubwa ya wananchi wa Nyanguge ikiwemo upungufu wa maji safi na salama. Aliongeza, serikali imesha kamilisha mipango na kwa miaka mitano ijayo, shida hiyo haitakuwepo tena.

Mwishoni aliwanadi wagombea udiwani na ubunge wa eneo hilo na kuwaomba wananchi wakipigie kura Chama Cha Mapinduzi na wagombea wake wote.

No comments:

Post a Comment